Na Josephat Lukaza
Msanii wa Muziki wa Dansi anayejulikana kama Christian Bella anayetamba na kibao chake cha Nani Kama Mama ni Mmoja wa Wasanii watakaotoa Burudani ya Kufa mtu katika Ukumbi wa Mlimani City Siku ya Jumamosi Tarehe 30 katika Fainali kubwa ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT).
Bella Amehaidi kutoa Burudani ya uhakika ambapo wapenzi wa muziki wake watafurahi na kufurahishwa na show atakayoitoa siku hiyo katika Fainali ya Kumkabidhi Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) kitita cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania.
Katika Fainali hiyo inayotarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Siku ya Jumamosi tarehe 30 huku viingilio vya Kuja kutazama fainali ya Kwanza kubwa vikiwa ni V.I.P Shilingi 50,000 na Kawaida 30,000 huku fainali hiyo ikirushwa live kupitia Kituo cha Runinga cha ITV na milango itakuwa wazi kuanzia Saa 7.30 Usiku.