Pages

Tuesday, June 3, 2014

CHUO CHA USAFIRISHAJI KUADHIMISHA VIPAJI KWA TAMASHA LA BURUDANI




CHUO cha Usafirishaji kilichopo jijini Dar es Salaam, kinatarajiwa kuadhimisha siku ya vipaji chuoni hapo ambapo mambo mbalimbali yatafanyika kusindikiza siku hiyo maalum chuoni hapo. Baadhi ya matukio yatakayofanyika ni pamoja na michezo kama soka, netiboli na kuvuta kamba. Vile vile burudani mbalimbali kama fashion show, muziki na vikundi vya kudansi vitakuwepo.
Tamasha hilo litakuwa na matukio mchanganyiko ya kielimu, michezo na burudani ambapo katika taaluma kutakuwa na hotuba za uhamasishaji, utengenezaji wa filamu na mengineyo.  Kwa upande wa michezo kutakuwa na mechi za soka ambapo Kitengo cha Manunuzi (Procurement) kitapambana na Kitengo cha Usafirishaji (Logistics)
Tamasha hilo pia litahusisha uchangiaji wa damu kupitia mradi wa ‘Damu Salama’ 

No comments:

Post a Comment