Pages

Monday, April 21, 2014

PICHA::CHEGE,YP WALIVYOWASHA MOTO COCO BEACH.




Msanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya Msomi John a.k.a War killer akiwapagawisha wakazi wa jiji la Dar es Salaam katika Tamasha la Cheka Bombastik lililoandaliwa na Vodacom Tanzania mahususi kwa ajili ya wateja wake katika msimu huu wa sikukuu ya pasaka na kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika fukwe za bahari ya hindi coco beach.

Mwanaidi Jumanne akiwa kwenye Swagga la ukweli la pasaka katika Tamasha la Cheka Bombastik lililoandaliwa na Vodacom Tanzania mahususi kwa ajili ya wateja wake katika msimu huu wa sikukuu ya pasaka na kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika fukwe za bahari ya hindi.

Msanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya Amir Jabir mkazi wa Namanga jijini Dar es Salaam akiwapagawisha wakazi wa jiji la Dar es Salaam kwenye Tamasha la Cheka Bombastik lililoandaliwa na Vodacom Tanzania mahususi kwa ajili ya wateja wake katika msimu huu wa sikukuu ya pasaka na kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika fukwe za bahari ya hindi.

Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya wa kundi la TMK Family Chege akiwapagawisha wakazi wa jiji la Dar es Salaam kwenye Tamasha la Cheka Bombastik lililoandaliwa na Vodacom Tanzania mahususi kwa ajili ya wateja wake katika msimu huu wa sikukuu ya pasaka na kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika fukwe za bahari ya hindi coco beach.

Nyomi ya watu iliyofurika kwenye Tamasha la Cheka Bombastik lililoandaliwa na Vodacom Tanzania mahususi kwa ajili ya wateja wake katika msimu huu wa sikukuu ya pasaka na kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika fukwe za bahari ya hindi jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam,  Katika kusheherekea sikuu ya Pasaka, wasanii Chege Chigunda au mtoto wa Mama Saidi na mwenzake YP wametoa burudani ya aina yake kwa wakazi wa Dar es Salaam katika tamasha maalum la Cheka Bombastik lililofanyika katika fukwe za Coco jijini Dar es Salaam.
Burudani ilianza kwa staili ya aina yake kwa wasanii Chipukizi “Underground” kupanda jukwaani na kutoa burudani kwa maelfu ya mashabiki waliojitokeza katika fukwe hizo.
Uwanja ulikuwa hautoshi pale alipopanda jukwaani Chege Chigunda na kuwapeleka Mashabiki wake Uswazi Take Away, kwa kuifanya kazi yake vyema na kutoa burudani ya Kipekee kwa pamoja  waliimba nyimbo kadhaa za kundi la Wanaume Family.
Akizungumza na waandishi wa habari punde baada ya kumalizika kwa Tamasha hilo, Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, ambao ndio waandaaji wa Tamasha hilo, Matina Nkurlu amesema kuwa Imekuwa kawaida kwa kampuni yao kutoa burudani kwa Wakazi wa Dar es Salaam na Sehemu nyingine katika ziku za siku kuu.
“Umekuwa ni Utaratibu wetu wa kawaida wa kutoa burudani kwa Watanzania ambao wamekuwa wakituunga mkono siku zote na kutufanya kuwa namba moja kila siku,” alisema Nkurlu na kuongeza, Umati huu ni ishara tosha ya namna wakazi wa Dar es Salaam walivyo kubali burudani hii”
“Burudani hii ni Maalum kwa wale wote ambao wanapenda kupumzika katika sehemu za Fukwe kama Coco Beach, tunatambua kuwa kipindi hiki wengi wanapenda kupumzika na familia zao hivyo ni vyema pia wakapata burudani ya aina hii.” Alisema Nkurlu.
Meneja huyo alisema kuwa burudani hiyo ni ya siku mbili, siku ya tarehe 20 na 21 ya Mwezi April ambayo ni jumapili na jumatatu ya pasaka, na wateja wa Vodacom watakao jitokeza katika Tamasha hilo, watapata zawadi mbalimbali na wataunganishwa na huduma ya Cheka Bombastik Bure, Ili kuweza kupiga simu kwa bei nafuu.
“Tumefanya Tamasha hili tukiwa na ujumbe maalum kwa wateja wetu wa Vodacom kuhakikisha wanajiunga na huduma yetu ya Cheka Bombastik ambayo inawapa nafasi ya kuchagua bando za aina mbali mbali za kupiga simu, Vodacom kwenda Vodacom au kutoka Vodacom kwenda mitandao mingine.”  Alihitimisha Nkurlu.

No comments:

Post a Comment